Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
64 1 Sikia sauti yangu, Baba yangu, katika kilio changu; uilinde nafsi yangu na hofu ya adui. 2 Unifiche na mashauri ya siri ya waovu, na kelele za kundi la watendao maovu. 3 Huinoa ndimi zao kama upanga; huelekeza maneno yao machungu kama mishale, 4 ili wampige kutoka mahali pa kuvizia yule asiye na hatia; humpiga ghafula pasipo hofu. 5 Hujitia nguvu katika kusudi lao ovu; huzungumza juu ya kuficha mitego nao husema, "Ni nani atakayeiona?"
6 Hupanga dhuluma, nao husema, "Tumekamilisha mpango uliobuniwa vyema." Fikira za ndani na moyo wa mwanadamu ni vya kina. 7 Lakini Baba yetu atawapiga kwa mshale; watajeruhiwa ghafula. 8 Watakwazwa; ndimi zao wenyewe zitageuka dhidi ya wao; wote watakaowaona watatikisa vichwa vyao.
9 Ndipo kila mtu ataogopa; watatangaza kazi ya Baba yetu na kutafakari aliyoyatenda. 10 Mwenye haki na afurahi katika Baba yetu na kukimbilia kwake; wote walio na moyo mnyofu na wapige kelele kwa furaha!