Ukimya Uliojaa Sifa
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.
65 1 Sifa yakungoja katika ukimya, Baba yetu, huko Sayuni; nawe utatimiziwa nadhiri zetu.
2 Wewe wasikia maombi, na watu wote watakuja kwako. 3 Dhambi zilip_nizidi nguvu, wewe uliyafunika makosa yetu. a a v3 Msamaha ambao Baba yetu autoao hapa hukamilika katika Yesu, aliyejitwika makosa yetu ili tuweze kurudishwa nyumbani. 4 Heri mtu yule umchaguaye na kumkaribisha akae nyua zako. Tutashiba wema wa nyumba yako, utakatifu wa hekalu lako.
5 Watujibu kwa matendo ya kutisha ya haki, Baba yetu utuokoaye, tumaini la miisho yote ya dunia na la bahari zilizo mbali kabisa. 6 aliyeziimarisha milima kwa nguvu zake, akivikwa uweza; 7 atulizaye ngurumo za bahari, ngurumo za mawimbi yake, na ghasia za mataifa. 8 Wakaao miisho ya dunia huzishangaa ishara zako za ajabu; wafanya mapambazuko na machweo kupaza sauti kwa furaha.
9 Waitunza nchi na kuinywesha ; waitajirisha kwa wingi. Mto wa Baba yetu umejaa maji; wawapa watu nafaka yao, kwa maana ndivyo ulivyoiandaa nchi. 10 Waikinaisha mifereji yake na kuisawazisha migongo yake; waililainisha kwa manyunyu na kuibariki mimea yake. 11 Waivika mwaka taji la wema wako, na njia zako hufurika neema tele. 12 Malisho ya jangwani hufurika, na vilima vimevikwa furaha. 13 Mabustani yamevikwa makundi ya wanyama na mabonde yamefunikwa nafaka; hupaza sauti kwa furaha na kuimba pamoja.