Hakuna Atendaye Mema
Kwa mwimbishaji. Mahalathi. Utenzi wa hekima wa Daudi.
53 1 Mpumbavu husema moyoni mwake, "Hakuna Mungu." Wameharibika, wakitenda uovu wa kuchukiza; hakuna atendaye mema.
2 Baba yetu alitazama chini kutoka mbinguni juu ya wanadamu wote ili aone kama yupo aelewaye, yupo amtafutaye. 3 Wote wamepotoka; kwa pamoja wameharibika; hakuna atendaye mema, hata mmoja.
4 Je, watenda uovu hawana maarifa — wale wawalao watu wangu kama walavyo mkate, wala hawamwiti Baba yetu? 5 Huko waliingiwa na hofu kuu, mahali ambapo hapakuwa na cha kuhofiwa; kwa maana Baba yetu aliitawanya mifupa yake yeye aliyepiga kambi juu yako; uliwaaibisha, kwa maana Baba yetu amewakataa.
6 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni! Baba yetu atakapowarudishia watu wake mafanikio yao, Yakobo na afurahi, Israeli na ashangilie.