Kilio cha Daudi cha Kuomba Wokovu
Kwa mwimbishaji. Kwa vinanda. Utenzi wa hekima wa Daudi, wakati Wazifi walipomwendea Sauli na kumwambia, “Je, Daudi hajifichi kati yetu?”
54 1 Ee Baba yangu, uniokoe kwa jina lako, unitetee kwa uweza wako. 2 Ee Baba yangu, usikie maombi yangu; uyasikilize maneno ya kinywa changu. 3 Kwa maana wageni wameinuka juu yangu, na wenye jeuri wanataka kuniua — hawamjali Baba yetu. Sela.
4 Hakika Baba yangu ni msaidizi wangu; Baba Mwenyezi ndiye antegemezaye uhai wangu. 5 Atawarudishia uovu wale wanaonivizia; kwa uaminifu wako, uwakomeshe. 6 Kwa sadaka ya hiari nitatoa dhabihu kwako; nitalisifu jina lako, Baba yangu, kwa kuwa ni jema. 7 Kwa maana ameniokoa katika kila taabu, na jicho langu limewatazama adui zangu kwa ushindi.