Vitu Vyote Ni Vyake
Zaburi ya Daudi.
24 1 Nchi ni ya Baba yetu, na vyote vilivyomo, ulimwengu, na wote wakaao ndani yake. 2 Kwa maana aliiweka misingi yake juu ya bahari na kuijenga juu ya mito. 3 Ni nani atakayepanda mlima wa Baba yetu? Naye ni nani atakayesimama mahali pake patakatifu? 4 Mtu mwenye mikono safi na moyo mweupe, asiyeuelekeza moyo wake katika ubatili, wala kuapa kwa hila. 5 Yeye atapokea baraka kutoka kwa Baba yetu, na haki kutoka kwa Baba yake amwokoaye. 6 Hicho ndicho kizazi cha wale wamtafutao, wautafutao uso wako, Ee Baba wa Yakobo. Sela. a a v6 Sela: yaelekea ni dokezo la muziki au kituo cha kutafakari wakati wa ibada; pia katika mstari wa 10.
7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango! Inukeni, enyi milango ya kale, ili Mfalme wa utukufu apate kuingia. 8 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? Ni Baba yetu, mwenye nguvu na uweza, Baba yetu, mwenye uweza vitani. b b v8 Mfalme wa utukufu aingiaye malangoni ni Baba yetu mwenyewe, mwenye nguvu za kuokoa na uweza wa kuwalinda watoto wake. 9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango! Inueni, enyi milango ya kale, ili Mfalme wa utukufu apate kuingia. 10 Ni nani huyu, Mfalme wa utukufu? Ni Baba wa majeshi ya mbinguni — yeye ndiye Mfalme wa utukufu. Sela.