Baba Yangu, Mchungaji Wangu
Zaburi ya Daudi.
23 1 Baba yangu ndiye mchungaji wangu; sitapungukiwa na kitu. 2 Katika malisho ya majani mabichi ananilaza; kando ya maji matulivu ananiongoza. 3 Huniburudisha nafsi yangu; huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4 Hata nikipita katika bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami; fimbo yako na mkongojo wako vyanifariji. 5 Waandaa meza mbele yangu machoni pa adui zangu; umenipaka kichwa changu mafuta; kikombe changu kinafurika. 6 Hakika wema na upendo usiokoma vitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa Baba yangu milele.