Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
13 1 Hata lini, Baba yangu, utanisahau? Hata milele? Hata lini utanificha uso wako?
2 Hata lini nitashindana na mawazo yangu na kubeba huzuni moyoni mwangu mchana kutwa? Hata lini adui yangu atanishinda? 3 Nitazame unijibu, Baba yangu; uyatie nuru macho yangu, nisije nikalala usingizi wa mauti.
4 Adui yangu atasema, "Nimemshinda," na watesi wangu watafurahi nianguapo. 5 Bali mimi nimeutumaini upendo wako thabiti; moyo wangu utafurahi katika wokovu wako. 6 Nitamwimbia Baba yangu, kwa kuwa amenitendea mema sana.