Kuenenda Katika Njia Zake
Wimbo wa kwenda juu.
128 1 Heri kila mtu amheshimuye Baba yetu, aendaye katika njia zake.
2 Utakula matunda ya kazi ya mikono yako; utabarikiwa, na mambo yatakwenda vema kwako. 3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; watoto wako kama miche ya mizeituni kuizunguka meza yako. 4 Tazama — hivyo ndivyo mtu amheshimuye Baba yetu atakavyobarikiwa.
5 Baba yetu akubariki kutoka Sayuni; upate kuuona ufanisi wa Yerusalemu siku zote za maisha yako, 6 tena upate kuwaona watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.