Wimbo wa Israeli wa Kunusurika
Wimbo wa kwenda juu.
129 1 "Wamenitesa sana tangu ujana wangu" — Israeli na aseme sasa — 2 "Wamenitesa sana tangu ujana wangu, lakini hawakunishinda." 3 Wakulima walilima juu ya mgongo wangu; wakafanya matuta yao marefu. 4 Baba yetu ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.
5 Wote wanaoichukia Sayuni na waaibishwe, warudishwe nyuma. 6 Na wawe kama majani ya juu ya nyumba, yanyaukayo kabla ya kukua, 7 ambayo mvunaji hajazi mkono wake, wala afungaye miganda kifua chake, 8 wala wapitao njiani hawasemi, "Baraka ya Baba yetu iwe juu yenu! Tunawabariki kwa jina la Baba yetu."