Yeye Asipoijenga
Wimbo wa kwenda juu. Wa Sulemani.
127 1 Baba yetu asipoijenga nyumba, waijengao wanajitaabisha bure. Baba yetu asipoulinda mji, mlinzi anakesha bure. 2 Ni bure kwenu kuamka mapema na kukesha usiku, mkila chakula cha taabu; kwa maana yeye humpa mpenzi wake usingizi.
3 Wana ni urithi utokao kwa Baba yetu, uzao wa tumbo ni thawabu. 4 Kama mishale mkononi mwa shujaa, ndivyo walivyo wana wa ujana. 5 Heri mtu aliyelijaza podo lake nao! Hataaibika atakapozungumza na adui zake langoni. a a v5 Lango la mji lilikuwa mahali pa hadhara ambapo migogoro ya kisheria na mambo ya jamii yalitatuliwa — kuwa na wana wengi kulimaanisha kuwa na watetezi wenye nguvu upande wako huko.