Soma. Pokea. Pendekeza.

♥ Maoni

Yohana 17

Kitabu

Baba, Saa Imefika

Chapter 17.

Baada ya kusema haya, Yesu akatazama juu mbinguni akasema: "Baba, saa imefika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana apate kukutukuza wewe," a a v1 Yohana 17 ni sala ndefu kuliko zote za Yesu kwa Baba zilizoandikwa — iliyonenwa usiku kabla ya msalaba, akiufungua moyo wake kwa Yule anayemwita Baba, Baba Mtakatifu, na Baba mwenye haki. kwa kuwa ulimpa mamlaka juu ya watu wote, ili awape uzima wa milele wale wote uliompa. Na uzima wa milele ndio huu: wakujue wewe, Baba wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi uliyonipa niifanye. Na sasa, Baba, unitukuze wewe pamoja nawe mwenyewe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.

Nimelidhihirisha jina lako kwa watu wale ulionipa kutoka katika ulimwengu. Walikuwa wako, ukanipa mimi, nao wamelishika neno lako. Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vyatoka kwako, kwa maana maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua kwa hakika ya kuwa nilitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ulinituma. Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu, bali wale ulionipa, kwa kuwa hao ni wako. Na vyote vilivyo vyangu ni vyako, na vyako ni vyangu; nami nimetukuzwa ndani yao. Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda kwa jina lako ulilonipa. Naliwatunza, wala hakupotea hata mmoja ila mwana wa uharibifu, ili Maandiko yapate kutimizwa. b b v12 "Mwana wa uharibifu" ni jina la Yuda Iskariote, yule aliyemsaliti Yesu. Na sasa naja kwako, nami nasema haya ulimwenguni ili wawe na furaha yangu imekamilika ndani yao. Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia kwa sababu wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu. Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu, bali uwalinde na yule mwovu. Wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu. Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. Kama wewe ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma wao ulimwenguni. Nami kwa ajili yao najitakasa mwenyewe, ili wao nao watakaswe katika kweli.

Wala si hawa peke yao ninaowaombea, bali na wale watakaoniamini kwa neno lao; Baba, wote wawe na umoja; kama wewe ulivyo ndani yangu, nami ndani yako, hao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ulinituma. Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilishwa katika umoja; tena ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi. Baba, nataka wale ulionipa wawe pamoja nami po pale nilipo, wapate kuutazama utukufu wangu ule ulionipa; kwa kuwa ulinipenda kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu. Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua wewe, lakini mimi nalikujua, na hawa wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma. Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo, ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.

A young man reading the Father's Heart Bible print edition in a coffee shop Sasa Imechapishwa

Maoni

Mawazo, maswali, au neno ambalo sura hii imeliamsha ndani yako — lishiriki hapa. Kila maoni huweka jina lako kwenye Wall of Contributors.

Kusoma, kunakili na kushiriki ni wazi kwa kila mtu — huhitaji akaunti. Kutoa maoni, kutia alama, na kuhifadhi mahali ulipofikia hupatikana kwa akaunti ya bure, na kila maoni huweka jina lako kwenye Wall of Contributors.

Jiunge na Familia — ni bure →
  • Bado hakuna maoni. Kuwa wa kwanza kuchangia.