Mzabibu na Mkulima
15 1 "Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. 2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda, yeye hulikata; na kila lizaalo matunda, hulisafisha, ili lizidi kuzaa matunda. 3 Ninyi tayari mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia. 4 Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda peke yake, lisipokaa katika mzabibu, kadhalika nanyi msipokaa ndani yangu. 5 Mimi ndimi mzabibu, ninyi ni matawi. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa matunda mengi, kwa maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote. 6 Mtu asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi na kunyauka; matawi hukusanywa, na kutupwa motoni, na kuteketea. 7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lo lote, nanyi mtatendewa. 8 Kwa njia hii Baba yangu hutukuzwa: ya kwamba mzae matunda mengi, na kudhihirika kuwa wanafunzi wangu.
9 Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi. Kaeni katika pendo langu. 10 Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu, kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu, na kukaa katika pendo lake. 11 Nimewaambia haya ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu iwe timilifu.
12 Amri yangu ndiyo hii: mpendane kama nilivyowapenda ninyi. 13 Hakuna aliye na pendo kubwa kuliko hili: mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. 14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo. 15 Siwaiti tena watumishi—kwa maana mtumishi hajui atendalo bwana wake. Bali nimewaita rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote niliyoyasikia kwa Baba yangu. a a v15 Yesu huwahamisha wanafunzi kutoka utumishi hadi urafiki kwa kushiriki nao yote aliyoyasikia kwa Baba yake — hii ndiyo shauku ya moyo wa Baba kwa kila msomaji, urafiki kupitia Mwana. 16 Si ninyi mlionichagua mimi—bali mimi naliwachagua ninyi, nikawaweka mwende mkazae matunda yadumuyo, ili lo lote mtakalomwomba Baba kwa jina langu, awape. 17 Haya nawaamuru, mpate kupendana.
Ulimwengu Utakapowachukia
18 "Ulimwengu ukiwachukia, jueni ya kuwa umenichukia mimi kabla yenu. 19 Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake. Lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu; bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia. 20 Likumbukeni lile neno nililowaambia: mtumishi si mkuu kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi pia; ikiwa walilishika neno langu, watalishika na lenu pia. 21 Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa sababu hawamjui yeye aliyenituma. 22 Kama nisingalikuja na kusema nao, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao. 23 Anichukiaye mimi humchukia na Baba yangu pia. 24 Kama nisingalitenda kwao kazi asizozitenda mtu mwingine, wasingalikuwa na dhambi. Lakini sasa wameona na kuchukia, mimi na Baba yangu pia. 25 Lakini hili limetokea ili litimie neno lililoandikwa katika torati yao: 'Walinichukia bure.'
26 "Ajapo yule Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba—huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba—yeye atanishuhudia." b b v26 Yule Msaidizi ambaye Yesu anaahidi ni Roho Mtakatifu — anayetumwa na Yesu kutoka kwa Baba, aitwaye hapa "Roho wa kweli" kwa sababu huwaongoza wanafunzi katika yote ambayo Yesu ameyadhihirisha.
27 Nanyi pia mnashuhudia, kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzo.