Wana wa Kora
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora.
85 1 Uliifadhili nchi yako, Baba yetu; uliwarejesha mateka wa Yakobo. 2 Uliusamehe uovu wa watu wako; ulizifunika dhambi zao zote. Sela. 3 Uliiondoa ghadhabu yako yote; ukaghairi hasira yako kali.
4 Uturejeshe, Baba yetu, wokovu wetu; uiondoe ghadhabu yako juu yetu. 5 Je, utatukasirikia milele? Utaiendeleza hasira yako vizazi vyote? 6 Je, hutatuhuisha tena, ili watu wako wafurahi kwako? 7 Tuonyeshe upendo wako wa agano, Baba yetu, na kutupa wokovu wako.
8 Nisikie yale Baba yetu atakayosema, kwa maana atawaambia watu wake amani, waaminifu wake; lakini wasirudi tena katika njia zao za upumbavu. 9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanaomcha yeye, ili utukufu ukae katika nchi yetu. 10 Upendo wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani zimebusiana. 11 Uaminifu unachipuka kutoka nchi, na haki inatazama chini kutoka mbinguni. 12 Naam, Baba yetu atatoa kilicho chema, na nchi yetu itatoa mavuno yake. 13 Haki itakwenda mbele yake na kuiandaa njia kwa hatua zake.