Jinsi Lilivyo Tukufu Jina Lako
Kwa mwimbishaji: mtindo wa Gitithi. Zaburi ya Daudi.
8 1 Ee Baba yetu Mwenye Enzi, jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Umeuweka utukufu wako juu ya mbingu. 2 Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umeuandaa uweza, kwa sababu ya watesi wako, ili kumnyamazisha adui na mlipiza kisasi. 3 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota ulizoziweka mahali pake, 4 mwanadamu ni kitu gani hata umkumbuke, naye mwana wa Adamu hata umwangalie? a a v4 Mwandishi wa Waebrania ayatumia maneno haya kwa Yesu — Mwana wa Adamu aliyefanywa mdogo kwa muda kidogo kuliko malaika, kisha akavikwa taji ya utukufu na heshima (Waebrania 2:6-9). 5 Lakini umemfanya mdogo kidogo kuliko viumbe vya mbinguni, ukamvika taji ya utukufu na heshima. 6 Umempa mamlaka juu ya kazi za mikono yako; umeweka vitu vyote chini ya miguu yake: 7 kondoo wote na ng'ombe, tena wanyama wa porini, 8 ndege wa angani, na samaki wa baharini, kila kipitacho njia za bahari. 9 Ee Baba yetu Mwenye Enzi, jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!