Ni nani apasaye kuwapo mbele zake?
Zaburi ya Daudi.
15 1 Baba, ni nani atakayekaa katika hema yako? Ni nani atakayeishi katika mlima wako mtakatifu? 2 Yeye aendaye kwa ukamilifu na kutenda haki, anenaye kweli kutoka moyoni mwake. 3 Hasingizii kwa ulimi wake, hamtendei jirani yake mabaya, wala hamsengenyi rafiki yake. 4 Humdharau mtu mbaya, bali huwaheshimu wamchao Baba yetu; hushika kiapo chake hata kimletee hasara, wala harudi nyuma. 5 Hakopeshi fedha yake kwa riba, wala hapokei rushwa juu ya asiye na hatia. Afanyaye mambo haya hataondoshwa milele.