Haleluya
146 1 Haleluya! Ee nafsi yangu, umsifu Baba yetu.
2 Nitamsifu Baba yetu maadamu ninaishi; nitamwimbia Baba yetu maadamu ninao pumzi.
3 Msiwatumainie wakuu, wala mwanadamu asiyeweza kuwaokoa. 4 Roho yake hutoka, hurudi ardhini; siku ile ile mawazo yake hupotea. 5 Heri mtu ambaye msaidizi wake ni Baba wa Yakobo, ambaye tumaini lake ni kwa Baba yetu,
6 Yeye ndiye Muumba wa mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo; hushika uaminifu milele. 7 Huwatendea haki walioonewa; huwapa chakula wenye njaa. Baba yetu huwaweka huru wafungwa. 8 Baba yetu huyafumbua macho ya vipofu; Baba yetu huwainua walioinama; Baba yetu huwapenda wenye haki. 9 Baba yetu huwalinda wageni; huwategemeza yatima na mjane, bali njia ya waovu huipindua.
10 Baba yetu atatawala milele — Baba yako, ee Sayuni, vizazi vyote. Haleluya!