Daudi Analia Kutoka Pangoni
Zaburi ya hekima ya Daudi, alipokuwa pangoni. Maombi.
142 1 Kwa sauti yangu namlilia Baba yangu; kwa sauti yangu namsihi anihurumie. a a v1 Maskili ni wimbo wa mafundisho wa kutafakari—zaburi iliyokusudiwa kutafakariwa, si kuimbwa tu. 2 Namimina malalamiko yangu mbele zake; mbele zake naeleza shida yangu. 3 Roho yangu inapozimia ndani yangu, ni wewe ujuaye njia yangu. Katika njia niendayo wamenifichia mtego. 4 Tazama upande wangu wa kuume uone — hakuna anayenitambua; hakuna kimbilio lililobaki kwangu; hakuna anayeijali nafsi yangu. 5 Nakulilia wewe, Baba yangu; nasema, "Wewe ndiwe kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai." 6 Sikiliza kilio changu, kwa maana nimeshushwa chini sana. Niokoe na wale wanaonifuata kwa maana wana nguvu mno kwangu. 7 Itoe nafsi yangu gerezani, ili nilishukuru jina lako. Wenye haki watanikusanyikia kwa maana utanitendea mema mengi.