Mtego Umevunjika
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
124 1 Kama Baba yetu asingekuwa upande wetu—Israeli na aseme sasa— 2 kama Baba yetu asingekuwa upande wetu watu walipoinuka kupigana nasi, 3 ndipo wangalitumeza tukiwa hai, hasira yao ilipowaka juu yetu; 4 ndipo maji yangalitufunika, kijito kingalipita juu yetu; 5 ndipo maji yenye ghadhabu yangalipita juu yetu.
6 Ahimidiwe Baba yetu, ambaye hakututoa tuwe mawindo ya meno yao! 7 Tumeokoka kama ndege kutoka mtego wa wawindaji; mtego umevunjika, nasi tumeokoka! 8 Msaada wetu u katika jina la Baba yetu, aliyeziumba mbingu na nchi.