Macho Yainuliwa Kuelekea Mbinguni
Wimbo wa kwenda juu.
123 1 Kwako wewe nainua macho yangu, wewe uketiye katika kiti cha enzi mbinguni. 2 Tazama — kama macho ya watumishi yamgeukiavyo mkono wa bwana wao, kama macho ya kijakazi kwa mkono wa bibi yake, ndivyo macho yetu yamgeukiavyo Baba yetu, hata atakapotufadhili. 3 Utufadhili, Baba yetu, utufadhili, kwa maana tumeshiba dharau kupita kiasi. 4 Nafsi yetu imeshiba kupita kiasi dhihaka za wale walio na raha, na dharau za wenye kiburi.