Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
122 1 Nalifurahi pamoja na wale waliosema kwangu, "Na twende nyumbani kwa Baba yetu." 2 Miguu yetu inasimama ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu. 3 Yerusalemu, uliojengwa kama mji ulioshikamana pamoja imara, 4 ambako makabila hupanda, makabila ya Baba yetu, kama amri kwa Israeli, kulishukuru jina la Baba yetu. 5 Kwa maana huko viti vya enzi vya hukumu viliwekwa, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
6 Iombeeni Yerusalemu amani: "Wapate raha wale wakupendao. 7 Amani iwe ndani ya kuta zako, salama ndani ya ngome zako." 8 Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu, nitasema, "Amani iwe ndani yako." 9 Kwa ajili ya nyumba ya Baba yetu nitakutafutia mema.