Wimbo wa kwenda juu.
120 1 Katika dhiki yangu nalimwita Baba yetu, naye akanijibu.
2 Baba yangu, niokoe na midomo ya uongo, na ulimi wa hila. 3 Baba yetu atakupa nini, tena ataongeza nini zaidi kwako, ewe ulimi wa hila? 4 Ya shujaa, mishale mikali, pamoja na makaa ya moto ya mretemu. a a v4 Mretemu ni kichaka cha jangwani ambacho makaa yake huwaka kwa joto kali na kwa muda mrefu sana.
5 Ole wangu, kwamba ninakaa Mesheki, kwamba ninafanya makao kati ya hema za Kedari! b b v5 Mesheki ilikuwa mbali kaskazini na Kedari mbali kusini-mashariki katika jangwa la Uarabuni — mahali palipo katika ncha mbili zilizo kinyume za ulimwengu uliojulikana, palipotajwa pamoja kuonyesha maisha ya kuzungukwa na wageni wenye uadui. 6 Nimekaa muda mrefu mno kati ya hao wachukiao amani. 7 Mimi ni wa amani; lakini ninenapo, wao ni wa vita.