Israeli Watoka Misri
114 1 Israeli alipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni, 2 Yuda likawa patakatifu pa Baba yetu, Israeli ukawa ufalme wake.
3 Bahari iliona, ikakimbia; Yordani ikarudi nyuma. 4 Milima iliruka-ruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 Una nini, ee bahari, hata ukakimbia? Una nini, ee Yordani, hata ukarudi nyuma? 6 Mna nini, enyi milima, hata mkaruka-ruka kama kondoo dume? Nanyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Tetemeka, ee nchi, mbele za uso wa Baba Mwenyezi, mbele za uso wa Baba yetu wa Yakobo, 8 aliyeugeuza mwamba kuwa ziwa la maji, jiwe gumu kuwa chemchemi itiririkayo.