Pasipo Ufunuo
Kuhusu watawala, hasira na watoto. Wenye haki wanapostawi watu hufurahi, na waovu watawalapo watu huugua. Mpumbavu humwaga hasira yake yote, na mwenye haraka ya kunena ni mbaya kuliko mpumbavu. Pasipo ufunuo, watu huenda holela.
29 1Yeye ambaye hukaripiwa mara kwa mara lakini akakataa kusikia atavunjika ghafla, wala hatapona. 2Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi, lakini waovu watawalapo, watu huugua. 3Mtu apendaye hekima humfurahisha babaye, lakini rafiki wa makahaba hutapanya mali yake. 4Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, lakini yeye aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza. 5Mtu ambaye humsifusifu jirani yake hutandaza wavu kwa ajili ya miguu yake. 6Mtu mwovu hunaswa na dhambi yake mwenyewe, lakini mwenye haki huimba na kufurahi. 7Wenye haki hujali haki ya maskini, lakini waovu hawana ufahamu wa jinsi hiyo. 8Wenye mzaha huuwasha mji moto, lakini wenye hekima hutuliza hasira. 9Mtu mwenye hekima ashindanapo na mpumbavu mahakamani, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani. 10Wenye kiu ya damu humchukia mkamilifu na hutafuta kuwaua wanyofu. 11Mpumbavu humwaga hasira yake yote, lakini mtu mwenye hekima huizuia na kujituliza. 12Mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu. 13Maskini na mdhalimu wanafanana katika jambo hili: Baba yetu huyapa nuru macho ya wote wawili. 14Mfalme akiwahukumu maskini kwa unyofu, kiti chake cha enzi kitathibitika milele. 15Fimbo na neno la karipio hutoa hekima, lakini mtoto aliyeachwa apende avyo humwaibisha mama yake. 16Waovu wanapostawi, uovu hustawi, lakini wenye haki wataona anguko la waovu. 17Mrudi mwanao, naye atakupa amani; ataleta furaha moyoni mwako. 18Pasipo ufunuo, watu huenda holela, lakini heri yeye aishikaye sheria. 19Mtumishi hawezi kurudiwa kwa maneno peke yake; ijapokuwa anaelewa, hatatii. 20Je, wamwona mtu aliye mwepesi wa maneno yake? Kuna tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake. 21Ukimdekeza mtumishi tangu utoto, mwishowe atakuwa kama mrithi. 22Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, na mtu mkali wa moyo hutenda dhambi nyingi. 23Kiburi cha mtu humshusha chini, lakini mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima. 24Mshirika wa mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huisikia laana lakini hasemi neno. a a v24 'Laana' ni kiapo cha hadharani kinachomtaka kila aliyeshuhudia uhalifu ajitokeze na kutoa ushahidi. 25Kumwogopa mwanadamu huleta mtego, lakini yeyote amtumainiye Baba yetu hulindwa salama. 26Wengi hutafuta upendeleo wa mtawala, lakini haki ya mtu hutoka kwa Baba yetu. 27Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye haki, na mtu mnyofu ni chukizo kwa waovu.