Wimbo Mpya
Zaburi.
98 1 Mwimbieni Baba yetu wimbo mpya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu; mkono wake wa kuume na mkono wake mtakatifu vimemshindia wokovu. 2 Baba yetu amedhihirisha wokovu wake; amefunua haki yake mbele ya mataifa. 3 Ameukumbuka upendo wake wa agano na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli; miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Baba yetu.
4 Mpigieni Baba yetu kelele za shangwe, dunia yote; pazeni sauti kwa nyimbo za furaha na kuimba sifa. 5 Mwimbieni Baba yetu sifa kwa kinubi, kwa kinubi na sauti ya wimbo. 6 Kwa tarumbeta na sauti ya baragumu, mpigieni kelele za shangwe mbele ya Mfalme, Baba yetu.
7 Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; dunia na wote wakaao ndani yake. 8 Mito na ipige makofi; vilima na viimbe kwa furaha pamoja 9 mbele ya Baba yetu, kwa maana anakuja kuihukumu dunia. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, na mataifa kwa unyofu.