Utubariki na Uangaze
Kwa mwimbishaji. Kwa vinanda. Zaburi. Wimbo.
67 1 Baba yetu na atufadhili na kutubariki, na kuangaza uso wake juu yetu. Selah a a v1 Selah: alama ya kituo cha kimuziki au kiliturujia; maana yake hasa haijulikani. 2 ili njia zako zijulikane duniani, wokovu wako kati ya mataifa yote. 3 Watu na wakusifu, Baba yetu; watu wote na wakusifu. 4 Mataifa na yafurahi na kuimba kwa shangwe, kwa maana wewe utawahukumu watu kwa haki, na kuyaongoza mataifa duniani. Selah
5 Watu na wakusifu, Baba yetu; watu wote na wakusifu. 6 Nchi imetoa mavuno yake; Baba yetu, Baba yetu mwenyewe, atubariki. 7 Baba yetu na atubariki, nayo miisho yote ya dunia imche.