Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
20 1 Baba yetu na akujibu siku ya taabu; jina la Baba wa Yakobo na likulinde. 2 Na akuletee msaada kutoka patakatifu, na akutegemeze kutoka Sayuni. 3 Na azikumbuke sadaka zako zote, na aitazame kwa upendeleo sadaka yako ya kuteketezwa. Sela. 4 Na akupe haja ya moyo wako, na atimize mashauri yako yote.
5 Tutashangilia kwa furaha kwa sababu ya wokovu wako, na kwa jina la Baba yetu tutainua bendera zetu. Baba yetu na atimize maombi yako yote. 6 Sasa ninajua ya kuwa Baba yetu humwokoa mpakwa mafuta wake; humjibu kutoka mbinguni kwake kutakatifu kwa nguvu ya wokovu ya mkono wake wa kuume. 7 Wengine hutumaini magari ya vita na wengine farasi, bali sisi tunalitumaini jina la Baba yetu. 8 Wao huanguka na kubwaga chini, bali sisi tunainuka na kusimama imara. 9 Baba yetu, mwokoe mfalme! Tujibu tunapokuita.