Mtoto Aliyetulia
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
131 1 Baba yangu, moyo wangu hauna kiburi, wala macho yangu hayajainuliwa; Sijishughulishi na mambo makuu na ya ajabu yaliyonizidi. 2 Hakika nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu, kama mtoto aliyeachishwa ziwa kwa mamaye; nafsi yangu ndani yangu i kama mtoto aliyeachishwa ziwa. 3 Ee Israeli, weka tumaini lako kwa Baba yetu, tangu sasa hata milele.