Amevikwa Utukufu
93 1 Baba yetu anatawala; amevikwa utukufu. Baba yetu amevikwa; amejifunga nguvu. Naam, ulimwengu umewekwa imara; hautaondoshwa kamwe. 2 Kiti chako cha enzi kimesimama tangu zamani za kale; wewe ni wa milele. 3 Mafuriko yameinuka, Baba yetu; mafuriko yamepaza sauti yao; mafuriko yanainua mawimbi yao yanayonguruma. 4 Mwenye nguvu kuliko ngurumo za maji mengi, mwenye nguvu kuliko mawimbi ya bahari, Baba yetu aliye juu ni mwenye nguvu. 5 Sheria zako ni thabiti sana; utakatifu unaipamba nyumba yako, Baba yetu, milele na milele.