Kilio Kutoka Miisho ya Dunia
Kwa mwimbishaji; kwa vinanda. Zaburi ya Daudi.
61 1 Sikia kilio changu, Baba yangu; sikiliza maombi yangu. 2 Toka miisho ya dunia nakuita, moyo wangu unapozimia; niongoze kwenye mwamba ulio juu kuliko mimi. 3 Kwa maana wewe umekuwa kimbilio langu, mnara imara dhidi ya adui.
4 Ninatamani kukaa katika hema yako milele na kujificha katika uvuli wa mbawa zako. Sela 5 Kwa maana wewe, Baba yangu, umesikia nadhiri zangu; umenipa urithi wa wale walichao jina lako. 6 Uziongeze siku za mfalme; miaka yake na idumu vizazi vingi. 7 Na akae katika kiti cha enzi mbele za Baba yetu milele; amuru upendo wako wa agano na uaminifu vimlinde. 8 Ndipo nitakapoliimbia sifa jina lako daima na kutimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.