Kwa mwimbishaji. Kwa vinanda. Zaburi ya Daudi.
4 1 Unijibu niitapo, Ee Baba yangu, wewe uitegemezaye haki yangu. Katika dhiki yangu ulinipa nafasi ya kupumua; unifadhili na uisikie sala yangu. 2 Enyi watu, hata lini heshima yangu itageuzwa kuwa aibu? Hata lini mtapenda maneno matupu na kufuatia uongo? Sela a a v2 Sela: alama ya kimuziki au ya kiibada katika zaburi; maana yake hasa haijulikani, lakini yaelekea inaashiria kituo au kipindi cha muziki.
3 Lakini jueni ya kuwa Baba yetu amejitengea yule mwaminifu; Baba yetu husikia nimwitapo. 4 Tetemekeni, wala msitende dhambi; yachunguzeni mioyo yenu vitandani mwenu, na mnyamaze. Sela
5 Toeni dhabihu za haki, na kumtumaini Baba yetu. 6 Wengi husema, "Ni nani atakayetuonyesha jambo lo lote jema?" Ee Baba yetu, tuinulie nuru ya uso wako!
7 Umetia furaha iliyo nyingi zaidi moyoni mwangu kuliko waliyo nayo wakati nafaka yao na divai yao mpya vinapozidi. 8 Kwa amani nitajilaza na kulala usingizi, kwa maana wewe peke yako, Ee Baba yangu, wanijalia kukaa salama.