Mwamba Wangu, Usinyamaze
Zaburi ya Daudi.
28 1 Kwako, Baba yangu, ninalia; Mwamba wangu, usiwe kiziwi kwangu, kwa maana ukinyamaza kimya kwangu, nitakuwa kama wale washukao shimoni.
2 Usikie sauti ya dua zangu za rehema nikuliliapo msaada, ninaponyanyua mikono yangu kuelekea patakatifu pako.
3 Usiniburute pamoja na wabaya, pamoja na watendao maovu, wanaosema maneno ya urafiki na jirani zao hali uovu umo mioyoni mwao. 4 Uwalipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na ubaya wa vitendo vyao; uwalipe sawasawa na kazi ya mikono yao; uwarudishie wanayostahili. 5 Kwa sababu hawajali kabisa kazi za Baba yangu wala kazi ya mikono yake, atawabomoa wala hatawajenga tena.
6 Ahimidiwe Baba yetu, kwa maana amesikia sauti ya dua zangu za rehema. 7 Baba yangu ni nguvu zangu na ngao yangu; moyo wangu umemtumaini, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha, nami kwa wimbo wangu nitamshukuru.
8 Baba yangu ni nguvu za watu wake; yeye ni ngome ya wokovu kwa masihi wake. 9 Uwaokoe watu wako, uubariki urithi wako; uwachunge na kuwachukua milele.