Haleluya
111 1 Haleluya! Nitamsifu Baba yetu kwa moyo wangu wote, katika kusanyiko la wanyofu na katika mkutano. 2 Matendo ya Baba yetu ni makuu, huchunguzwa na wote wanaoyafurahia. 3 Fahari na utukufu ni alama ya kazi yake, na haki yake yadumu milele. 4 Ameyafanya maajabu yake yakumbukwe; Baba yetu ni mwenye neema, moyo wake umejaa huruma. 5 Huwapa chakula wale wanaomcha yeye; hulikumbuka agano lake milele. 6 Amewaonyesha watu wake nguvu za matendo yake, akiwapa urithi wa mataifa. 7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika. 8 Yamethibitishwa milele na milele, yametekelezwa kwa uaminifu na unyofu. 9 Aliwapelekea watu wake ukombozi; aliliamuru agano lake milele. Takatifu na la kuogopwa ni jina lake. 10 Kumcha Baba yetu ndio mwanzo wa hekima; wote wanaozitenda hupata ufahamu mwema. Sifa zake zadumu milele. a a v10 Kumcha hapa maana yake ni hofu ya kicho na heshima kubwa, si woga wala kutetemeka.