Njia Mbili, Miisho Miwili
1 1 Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki, wala hakusimama miongoni mwa wenye dhambi, wala hakuketi katika kiti cha wenye dhihaka. 2 bali furaha yake ni katika sheria ya Baba yetu, na sheria yake huitafakari mchana na usiku. 3 Naye atakuwa kama mti uliopandwa kandokando ya vijito vya maji, uzaao matunda yake kwa majira yake, wala jani lake halinyauki — na kila alitendalo litafanikiwa.
4 Sivyo walivyo wasio haki! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo. 5 Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki. 6 Kwa maana Baba yetu huilinda njia ya wenye haki, bali njia ya wasio haki itapotea.