Baba Yetu Anena
34 1Naye Baba yetu akanena na Musa, akisema,
2"waamuru Waisraeli: mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, hii ndiyo nchi itakayowaangukia kuwa urithi—nchi ya Kanaani, ndani ya mipaka yake. 3Upande wenu wa kusini utaanzia jangwa la Sini kandokando ya mpaka wa Edomu; mpaka wenu wa kusini utaanzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, upande wa mashariki. 4Mpaka wenu utageuka kuelekea kusini mwa Mwinuko wa Akrabimu, uvuke kwenda Sini, ufike kusini mwa Kadesh-barnea, uendelee mpaka Hasar-adari, na kupita hata Asmoni. 5Kutoka Asmoni mpaka utageuka kuelekea Kijito cha Misri, na kuishia baharini.
6"Mpaka wenu wa magharibi utakuwa Bahari ya Mediterania na pwani yake. a a v6 Bahari Kubwa ndiyo Bahari ya Mediterania.
7"Huu ndio utakaokuwa mpaka wenu wa kaskazini: kutoka Bahari ya Mediterania mtapiga mstari wenu hata Mlima Hori. 8Kutoka Mlima Hori mtapiga mstari hata Lebo-hamathi, na kuishia Sedadi; 9kisha mpaka utaenea hata Zifroni na kuishia Hasar-enani. Huu ndio utakaokuwa mpaka wenu wa kaskazini.
10"Mtachora mpaka wenu wa mashariki kutoka Hasar-enani hata Shefamu. 11Mpaka utateremka kutoka Shefamu hata Ribla, upande wa mashariki wa Aini, kisha utateremka na kufikia mteremko ulio mashariki mwa Bahari ya Kinerethi. b b v11 Bahari ya Kinerethi ndilo ziwa lililokuja kuitwa Bahari ya Galilaya. 12Mpaka utateremka hata Yordani, na kuishia katika Bahari ya Chumvi. Hii ndiyo itakayokuwa nchi yenu, pamoja na mipaka yake pande zote."
13Musa akawaamuru Waisraeli: Hii ndiyo nchi mtakayoirithi kwa kura, ambayo Baba yetu ameamuru kupewa kabila tisa na nusu ya kabila. 14Kabila la wana wa Reubeni, kwa nyumba za baba zao, na kabila la wana wa Gadi, kwa nyumba za baba zao, wamekwisha kupokea urithi wao; vivyo hivyo na nusu ya kabila la Manase. 15Kabila mbili na nusu wamepokea urithi wao ng'ambo ya Yordani kutoka Yeriko, upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua.
Baba Yetu Anena Tena
16Naye Baba yetu akanena na Musa, akisema,
17"haya ndiyo majina ya watu watakaowagawia nchi kuwa urithi: Eleazari kuhani na Yoshua mwana wa Nuni. 18Nanyi mtatwaa kiongozi mmoja kutoka kila kabila kwa kuigawanya nchi kuwa urithi. 19Haya ndiyo majina ya watu: kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune; 20kutoka kabila la wana wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi; 21kutoka kabila la Benyamini, Elidadi mwana wa Kisloni; 22kutoka kabila la wana wa Dani, kiongozi, Buki mwana wa Yogli; 23kutoka wana wa Yusufu: kutoka kabila la Manase, kiongozi Hanieli mwana wa Efodi, 24na kutoka kabila la wana wa Efraimu, kiongozi, Kemueli mwana wa Shiftani; 25kutoka kabila la wana wa Zabuloni, kiongozi, Elisafani mwana wa Parnaki; 26kutoka kabila la wana wa Isakari, kiongozi, Paltieli mwana wa Azani; 27kutoka kabila la wana wa Asheri, kiongozi, Ahihudi mwana wa Shelomi; 28na kutoka kabila la wana wa Naftali, kiongozi, Pedaheli mwana wa Amihudi."
29Hawa ndio ambao Baba yetu aliwaamuru kuwagawia urithi wana wa Israeli katika nchi ya Kanaani.