Siku ya Maangamizi kwa Misri
Wimbo wa kuomboleza juu ya Misri na washirika wake, ukitaja mji baada ya mji, Memfisi, Thebesi, Pelusiamu, Tahpanhesi, ikitiwa moto au kuchukuliwa mateka. Mkono wa Farao tayari umevunjwa na Baba yetu wala hautafungwa banzi, na upanga unatiwa katika mkono wa Babeli badala yake.
30 1Neno la Baba yetu likanijia:
2Mwana wa Adamu, tabiri na useme: Baba Mwenyezi asema hivi: "Ombolezeni, 'Ole wa siku ile!' 3Kwa maana siku ile i karibu, siku ya Baba yetu i karibu— siku ya mawingu, wakati wa maangamizi kwa mataifa. 4Upanga utakuja juu ya Misri, na uchungu utakuwa katika Kushi wakati waliouawa waangukapo Misri, wakati watakapochukua utajiri wake na misingi yake itakapobomolewa. 5Kushi, Puti, na Ludi, Arabia yote, Libya, na watu wa nchi ya agano wataanguka pamoja nao kwa upanga. 6Baba yetu asema hivi: "Wale wanaoiunga mkono Misri wataanguka, na nguvu zake za kiburi zitashuka; kutoka Migdoli hadi Aswani wataanguka ndani yake kwa upanga, asema Baba Mwenyezi. 7Watakuwa ukiwa kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake itakuwa kati ya miji iliyoharibiwa. 8Ndipo watakapojua ya kuwa mimi ndimi Baba, nitakapotia moto Misri na wasaidizi wake wote watakapovunjwavunjwa.
9Siku ile wajumbe watasafiri kwa merikebu kutoka kwangu ili kuwatia hofu Wakushi walio salama, na uchungu utawakamata katika siku ya Misri—kwa maana hakika inakuja.
10Baba Mwenyezi asema hivi: "Nitakomesha makutano ya Misri kwa mkono wa Nebukadneza mfalme wa Babeli. 11Yeye na jeshi lake pamoja naye, walio wakali kuliko mataifa yote, wataletwa ili kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi waliouawa. 12Nitaikausha mito ya Nili na kuiuza nchi kwa watenda maovu; nitaifanya nchi kuwa ukiwa, na vyote vilivyomo ndani yake, kwa mkono wa wageni. Mimi, Baba, nimenena."
13Baba Mwenyezi asema hivi: "Nitaziharibu sanamu na kukomesha vinyago visivyofaa kitu katika Memfisi. Hatakuwapo tena mkuu katika nchi ya Misri, nami nitaeneza hofu katika nchi yote. a a v13 Memfisi ulikuwa mji mkuu wa kale wa Misri ya Chini—katika Kiebrania cha Ezekieli unaitwa Nofu. 14Nitaifanya Pathrosi kuwa ukiwa, nitatia moto Soani, na kuleta hukumu juu ya Thebesi. b b v14 Thebesi ulikuwa mji mkuu wa Misri ya Juu—katika Kiebrania cha Ezekieli unaitwa No. 15Nitaimwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiamu, ngome ya Misri, na kuyakatilia mbali makutano ya Thebesi. 16Nitatia moto Misri; Pelusiamu itagaagaa kwa uchungu, Thebesi itabomolewa, na Memfisi itakabiliana na adui mchana. 17Vijana wa Heliopoli na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yenyewe itakwenda utumwani. 18Huko Tahpanhesi mchana utatiwa giza nitakapovunja nira ya Misri huko, na nguvu zake za kiburi zitafikia mwisho ndani yake. Wingu litaifunika, na miji yake ya binti zake itakwenda utumwani. 19Hivyo nitaleta hukumu juu ya Misri. Ndipo watakapojua ya kuwa mimi ndimi Baba."
Baba Anavunja Mkono wa Farao
20Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa kwanza, siku ya saba, neno la Baba yetu likanijia:
21Mwana wa Adamu, nimeuvunja mkono wa Farao mfalme wa Misri; haukufungwa ili upone wala kuwekewa banzi, upate kuwa na nguvu za kutosha kushika upanga. 22Basi Baba Mwenyezi asema hivi: "Mimi ni juu ya Farao mfalme wa Misri. Nitaivunja mikono yake—ile yenye nguvu na ile iliyovunjika—na kuufanya upanga uanguke kutoka mkononi mwake. 23Nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa na kuwatapanya katika nchi mbalimbali. 24Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli na kuutia upanga wangu mkononi mwake, lakini nitaivunja mikono ya Farao, naye Farao ataugua mbele ya mfalme wa Babeli kama mtu anayekufa. 25Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli, lakini mikono ya Farao itaanguka. Ndipo watakapojua ya kuwa mimi ndimi Baba, nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye atakapounyoosha juu ya nchi ya Misri. 26Nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa na kuwatapanya katika nchi mbalimbali. Ndipo watakapojua ya kuwa mimi ndimi Baba."