Soma. Pokea. Pendekeza.

♥ Maoni

2 Samweli 12

Kitabu

Baba yetu Amtuma Nathani kwa Daudi

Sura ya 12.

Baba yetu akamtuma Nathani kwa Daudi. Naye akaja akasema, "Palikuwa na watu wawili katika mji fulani, mmoja tajiri na mwingine maskini. Yule tajiri alikuwa na makundi mengi sana ya kondoo na ng'ombe, lakini yule maskini hakuwa na kitu ila mwana-kondoo mmoja mdogo aliyekuwa amemnunua. Akamlea, naye akakua pamoja naye na watoto wake. Alikula chakula sahanini pake, akanywa kikombeni pake, na kulala kifuani pake; alikuwa kama binti kwake. Msafiri mmoja akamjia yule tajiri, lakini yeye hakupenda kutwaa katika kondoo wake mwenyewe wala ng'ombe wake ili amwandalie mgeni aliyekuja. Basi akamtwaa mwana-kondoo wa yule maskini, akamwandalia yule mtu aliyemjia."

Daudi akawaka hasira kali sana juu ya mtu yule, akamwambia Nathani, "Kama aishivyo Baba yetu, mtu aliyefanya jambo hili astahili kufa! Ni lazima amrudishe mwana-kondoo mara nne, kwa sababu alifanya jambo hili wala hakuwa na huruma."

Ndipo Nathani akamwambia Daudi, "Wewe ndiwe mtu huyo! Baba yetu, Mungu wa Israeli, asema hivi: Mimi nalikutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli, nami nalikuokoa kutoka mkononi mwa Sauli.

"Nalikupa nyumba ya bwana wako, na wake zake kifuani mwako, na nyumba ya Israeli na ya Yuda. Na kama hayo yangelikuwa machache, ningelikuongezea zaidi tena na tena. Kwa nini umelidharau neno langu, ukafanya yaliyo maovu machoni pangu? Umempiga Uria, Mhiti, kwa upanga, ukamtwaa mkewe awe mke wako, ukamwua kwa upanga wa Waamoni. Basi sasa upanga hautaondoka nyumbani kwako milele, kwa sababu umenidharau mimi, ukamtwaa mkewe Uria, Mhiti, awe mke wako.

Baba yetu asema hivi: Tazama, nitakuinulia msiba kutoka nyumbani mwako mwenyewe. Nitawatwaa wake zako mbele ya macho yako, nami nitampa jirani yako, naye atalala nao wakati wa mchana peupe. Kwa maana wewe ulifanya jambo hilo kwa siri, bali mimi nitafanya jambo hili mbele ya Israeli wote, wakati wa mchana peupe."

Daudi akamwambia Nathani, "Nimemtenda Baba yetu dhambi." Nathani akamjibu, "Baba yetu naye ameiondoa dhambi yako; hutakufa."

Lakini kwa kuwa kwa tendo hili umemdharau sana Baba yetu, kwa hakika mtoto utakayezaliwa atakufa. Ndipo Nathani akaenda nyumbani kwake. Naye Baba yetu akampiga yule mtoto ambaye mkewe Uria alikuwa amemzalia Daudi, akaugua sana. Basi Daudi akamsihi Baba yetu kwa ajili ya yule mtoto. Daudi akafunga, akaingia ndani, akalala usiku kucha juu ya nchi. Wazee wa nyumba yake wakasimama karibu naye ili wamwinue toka nchi, lakini yeye akakataa, wala hakula chakula pamoja nao. Ikawa siku ya saba mtoto akafa. Watumishi wa Daudi wakaogopa kumwambia ya kuwa mtoto amekufa, kwa maana walisema, "Tazama, mtoto alipokuwa hai, tulisema naye, wala hakusikiliza sauti yetu. Tutamwambiaje basi ya kuwa mtoto amekufa? Huenda akajidhuru mwenyewe."

Lakini Daudi alipowaona watumishi wake wakinong'ona, akatambua ya kuwa mtoto amekufa. Basi Daudi akawauliza watumishi wake, "Je! Mtoto amekufa?" Wakamwambia, "Amekufa."

Ndipo Daudi akainuka toka nchi, akaoga, akajipaka mafuta, akabadili mavazi yake. Akaenda nyumbani mwa Baba yetu, akasujudu; kisha akarudi nyumbani kwake, na kwa amri yake wakamwandalia chakula, naye akala. Watumishi wake wakamwuliza, "Ni jambo gani hili ulilolitenda? Mtoto alipokuwa hai, ulifunga na kulia; naye alipokufa, umeinuka na kula chakula."

Akasema, "Mtoto alipokuwa hai, nalifunga na kulia; kwa maana nalisema, 'Ni nani ajuaye? Huenda Baba yetu akanifadhili, mtoto akaishi.' Lakini sasa amekufa; kwa nini nifunge? Je! Naweza kumrudisha tena? Mimi nitakwenda kwake, bali yeye hatanirudia mimi."

Kisha Daudi akamfariji mkewe Bathsheba, akaingia kwake, akalala naye; naye akazaa mwana wa kiume, akamwita jina lake Sulemani. Naye Baba yetu akampenda, akatuma neno kwa mkono wa Nathani nabii, naye akamwita jina lake Yedidia, kwa ajili ya Baba yetu. a a v25 Yedidia maana yake "mpendwa wa Baba yetu" — jina hili linaonyesha upendo ambao Baba yetu alikuwa ndipo ameuweka juu ya mtoto.

Daudi Auteka Raba

Wakati huo Yoabu akapigana na Raba wa Waamoni, akauteka mji wa kifalme. Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi, akasema, "Nimepigana na Raba, naam, nimeuteka mji wa maji. Basi sasa uwakusanye watu wa jeshi waliobaki, uupige kambi mji, uuteke; nisije nikautwaa mimi mji, ukaitwa kwa jina langu."

Basi Daudi akawakusanya watu wote wa jeshi, akaenda Raba, akaupiga vita, akauteka. Akaitwaa taji ya mfalme wao toka kichwani pake—ilikuwa na uzito wa ratili kama sabini na tano za dhahabu, na kito cha thamani ndani yake—nayo ikawekwa juu ya kichwa cha Daudi. Naye akatoa nyara nyingi sana mjini. Akawatoa watu waliokuwamo humo, akawaweka wafanye kazi kwa misumeno, na sululu za chuma, na mashoka ya chuma, akawatia kazini penye matanuru ya matofali. Ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote wa jeshi wakarudi Yerusalemu.

A young man reading the Father's Heart Bible print edition in a coffee shop Sasa Imechapishwa

Maoni

Mawazo, maswali, au neno ambalo sura hii imeliamsha ndani yako — lishiriki hapa. Kila maoni huweka jina lako kwenye Wall of Contributors.

Kusoma, kunakili na kushiriki ni wazi kwa kila mtu — huhitaji akaunti. Kutoa maoni, kutia alama, na kuhifadhi mahali ulipofikia hupatikana kwa akaunti ya bure, na kila maoni huweka jina lako kwenye Wall of Contributors.

Jiunge na Familia — ni bure →
  • Bado hakuna maoni. Kuwa wa kwanza kuchangia.